112 - AL - IKHLAS'

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU. 

 

1. Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee. 

2. Mwenyezi Mungu Mkusudiwa. 

3. Hakuzaa wala hakuzaliwa. 

4. Wala hana anaye fanana naye hata mmoja.